tangazo
Loading...

.

Serikali Haijazuia Watumishi Wa Umma Kukopa Benki


SeeBait
Kumekuwa na taarifa inasambazwa katika mitandao ya kijamii, makundi ya ‘WhatsApp’, ‘Facebook’ na majukwaa mbalimbali ikieleza kuwa Serikali imepiga marufuku watumishi wa umma kukopa Benki,SACCOS,VICOBA na Taasisi mbalimbali za kifedha.

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 20 Desemba 2016 na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeeleza kuwa taarifa inayosambazwa, ambayo imetafsiri mawasiliano ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni ya kupotosha, hivyo watumishi wote wa umma wanaombwa kuipuuza.

Vilevile watumishi wa umma wametakiwa kuzingatia kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali HAINA mamlaka ya kuzuia wala kuruhusu mtumishi yeyote wa Serikali kukopa au kutokopa katika Taasisi yoyote ya Fedha nchini.

Watumishi wa umma pia wamekumbushwa kuwa mikopo yote ya watumishi wa umma katika Taasisi za Fedha hutolewa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu zilizopo ili mradi mtumishi awe ametimiza vigezo.

Aidha, watumishi wa umma wameaswa kuacha tabia ya kusambaza taarifa zisizo za kweli na ambazo zina mamlaka husika ya kuzitoa ikiwa ni pamoja na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.
***
 

Advertisement

Ndalichako Asitisha Ajira za Walimu Wa Masomo ya Sanaa


WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, ametoa masharti mapya ya ajira za ualimu nchini, huku akisema Serikali haitaajiri walimu wa masomo ya sanaa (arts) kwa kuwa wapo wa kutosha.

Akizungumza mjini Dodoma jana wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA), Profesa Ndalichako, alisema Serikali kwa sasa haiwezi kuajiri walimu wa masomo hayo kwa kuwa inataka kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ambao idadi yao ni ndogo.

“Pamoja na uamuzi huo mpya, ajira za walimu wapya wa masomo ya sayansi nazo zimebadilika kwani wale wote waliohitimu ualimu wa sayansi na hisabati, wanatakiwa watume vyeti vyao kabla ya kupangiwa kituo cha kazi.

“Kuhusu wale walimu wa ‘arts’, kule tuna walimu wa ziada ambao tutajaribu kuwapanga kutokana na shule, kwani wengi walikuwa wamepangwa shule moja. Kwahiyo, tutaangalia utaratibu wa kuwapanga kulingana na mahitaji,’’ alisema Profesa Ndalichako.

Akizungumzia suala la ubora wa elimu nchini, Profesa Ndalichako aliwataka walimu wakuu hao kuhakikisha wanasimamia ubora wa elimu kwa kuwa wao ndio wanaowaandaa wanafunzi kabla hawajaenda vyuoni.

“Vilevile pelekeni takwimu sahihi za wanafunzi waliopo katika shule zenu kuisaidia Serikali katika kupanga bajeti ili iweze kutoa fedha sahihi.

“Hapa kuna kimbembe, yaani wakati mwingine huwa najifanya nimepoteza takwimu ya shule fulani, nikiziomba na kutumiwa, zinakuwa ni tofauti na zile za mwanzo.

“Hili nawaomba mkalisimamie ili iwe rahisi kwetu kupanga bajeti yenye tija,’’ alisema.

Kuhusu ujenzi wa maabara katika shule za sekondari, waziri huyo alisema kwamba kutokana na nyingi kukamilika, Serikali itatoa vifaa vya maabara kuanzia Januari mwakani baada ya kuwa vimeingia nchini kutoka vilikoagizwa.

Awali, akisoma risala ya walimu hao, Rais wa TAHOSSA, Bonus Nyimbo, aliiomba Serikali itoe waraka wa kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi shuleni kwa kuwa zimekuwa zikichangia kushuka kwa ufaulu kwa baadhi ya wanafunzi.

“Ili kuboresha elimu, tunaiomba Serikali itoe waraka wa kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi kwani simu nyingi tunazozikamata tunakuta mule hakuna taaluma,’’ alisema Nyimbo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Global Education Link, Abdulmalik Molel, ambaye pia kampuni yake ilipewa tuzo ya heshima katika kuendeleza elimu nchini, alisema ni jukumu la kila mmoja kutimiza wajibu wake ili kuiendeleza elimu ya Tanzania.

“Kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu, wazazi, walezi na walimu, waambieni wanafunzi wasiwe na ‘expectation’ (matarajio) makubwa kwani wanapokuwa na matarajio hayo, wakienda vyuo vikuu wanakuwa wasumbufu,” alisema.

Wakati hayo yakiendelea, juzi taarifa ilitolewa jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Maimuna Tarishi, ikisema kwamba, walimu wahitimu wa masomo ya sayansi na hisabati waliohitimu shahada na astashahada mwaka 2015, wanatakiwa kuwasilisha nakala za vyeti vya elimu ya sekondari vya kidato cha nne na sita na taaluma ya ualimu kwa uhakiki.

Pamoja na hayo, hivi karibuni Serikali ilitangaza kusitisha ajira zote nchini ili kukabiliana na wimbi la watumishi hewa.

Sambamba na uamuzi huo, nyongeza za mishahara kwa watumishi wa Serikali nazo zilisimamishwa ili kukabiliana na watumishi hao hewa ambao walikuwa wakiingizia hasara Serikali.

Waziri Mkuu Acharuka....Asema NGO Chonganishi Zitafutwa


SeeBait
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa miezi sita ya kujitathimini mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanayofanya kazi zake wilayani Ngorongoro mkoani Arusha, kama yanafanya kazi kwa misingi ya sheria na maadili.

Baadaye, yatahakikiwa na kama yatabainika yanachochea migogoro, yatafutwa.

Pia, Majaliwa amezicharukia NGOs nyingine zinazoitangaza vibaya Tanzania kimataifa kwa kupiga picha za kudhalilisha watoto wakiwa wanatembea kwenye mawe huku wamevaa kandambili kubwa, kuonesha nchi ni masikini. Ametaka NGOs hizo kuondoka nchini, la sivyo serikali itazishughulikia.

“Hizi NGOs zingine si muondoke, nendeni kwingine mkafanye kazi. Halafu nyie mnaotuma picha za kudhalilisha watoto wakiwa wamevaa kandambili kubwa, kudai nchi za nje eti Tanzania ni masikini, tutawashughulikia,” alisema Majaliwa alipozungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro jana.

Aidha alisema Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) atakuja wilayani hapo kukagua kazi walizozifanya, wanazozifanya na miradi wanaosaidia jamii.

Majaliwa aliwaambia watumishi hao wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo wakurugenzi wa mashirika yasiyo ya serikali, yanayofanya shughuli zake wilayani hapo, kuwa serikali haitaki mashirika chochezi wa migogoro na itayafuta.

Alisema serikali haitasita kuyafuta mashirika yanayofanya kazi wilayani humo, ambayo yapo kwa nia ya uchochezi na kuacha kufanya kazi katika malengo yaliyokusudiwa.

Waziri Mkuu alisema wilaya hiyo, ina mashirika yasiyo ya serikali 30 ambayo yamesajiliwa, lakini yanayofanya kazi ni 19 tu.

Alisisitiza kuwa haiwezekani serikali isajili mashirika hayo, lakini utendaji kazi wake uwe hafifu.

Alisema ukifuatilia, mashirika hayo utagundua kuwa yanapokea fedha nyingi, lakini hakuna cha maana wanachokifanya kwa wananchi. Alisema serikali ina taarifa ya NGOs hizo zinazopewa fedha na wafadhili.

“Najua taarifa zenu mnapokea kiasi gani cha fedha na mnazifanyia nini, lakini namleta Mkaguzi wa serikali ili akague mnatumiaje fedha zenu, nawapa miezi sita tu halafu ukaguzi utaanza, maana kuna mashirika mengi lakini kazi mnazofanya hazionekani,” alisema Majaliwa.

Alisema baadhi ya mashirika, yana akaunti nchi jirani ya Kenya na mengine kama PWC anapewa Sh bilioni 2.5 kwa mwaka na shirika la UCRT linapokea Sh bilioni 1.5 kwa mwaka, lakini hajui yanafanya nini.

“Nina taarifa zenu mnapata hela nyingi, lakini mnahudumia vipi jamii hakuna, sasa ngojeni ukaguzi ufanyike halafu nitachukua maamuzi maana kila siku Loliondo kuna nini hapa mnasajiliwa halafu hakuna cha maana,” alisema.

“Kuna nini Loliondo, kwani kila mara Loliondo nina taarifa za kila NGOs zinazofanya kazi hapa, najua mnachokifanya, sasa nawaambia serikali haitawafumbia macho kuona hiki ninachokifanya hapa na ikigundulika mnafanya kinyume na matakwa ya usajili tutazifuta”.

Alisema serikali itazifuta NGOs zote, ambazo zitabainika ni kiini cha migogoro Loliondo. Alitoa hadhari kwa kampuni zinazofanya kazi zake bila usajili, kuwa zikigundulika, zitachukuliwa hatua.

Aliwageukia watumishi wa umma na kuwatahadharisha wale wanaotoa taarifa za migogoro ya ndani kwa wahusika wa NGOs na kisha kuzituma nje ya nchi kwenye mitandao ya kijamii na barua pepe.

Alisema kuwa nao watashugulikiwa, kwa kuwa wanapaswa kuwa majibu ya migogoro na si wasambazaji wa habari mbaya za nchi.

Alisisitiza watekeleze kikamilifu kauli ya ‘Hapa Kazi Tu’ ; na si kutumia NGOs kwa ajili ya kudai kuwasaidia wananchi, huku wakijua kuwa wananchi hawanufaiki na fedha hizo wanazopewa na wafadhili Awali akizungumza na watumishi wa halmashauri ya Wilaya hiyo, Majaliwa alitoa tahadhari kwa madiwani kuacha kushirikiana na watu wa Uhasibu wanaotoa hela kwaajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema baadhi ya madiwani, wanakwamisha miradi ya maendeleo kwa kula fedha kwa sababu ya ukaribu walionao.

Akizungumzia nidhamu ya fedha, Majaliwa alisisitiza kila mtumishi lazima afanye kazi kwa bidii, ikiwemo kutoa huduma bila kuwabagua wananchi kwa itikadi zao za vyama.

Advertisement

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Disemba 16


SeeBait



Advertisement
Older Posts
© Copyright MCHANYATO | Designed By JIJI LETU
Back To Top